Kuchunguza athari ya lugha ya Kikonjo katika kujifunza lugha ya Kisawhili
Abstract
Lengo kuu la utafiti huu ni kujua jinsi ambavyo mtoto wa kikonzo anayejifunza lugha ya Kiswahili anavyoathiriwa na lugha yake ya mama katika harakati za kujifunza lugha ya kiswhili sanifu. Utafiti huu umefanywa katika mjini Kasese.Taasisi mbili zilishilikishwa kwa shule za sekondari kasese na Hima Green Hill. Pia wataaluma ( wazazi) wa vijiji hivyo Kasese na Hima.Utafiti huu umetumia mbinu ya dodoso, hojaji na mahojiano ya makundi katika kusanya data. Matokeo ya utafiti huu umebaini kwamba athari ya lugha ya kikonjo katika kujifunza lugha ya Kiswahili sanifu inatokana na sababu ya Watoto kuhamisha uelewa wa lugha ya kwanza ya
kikonjo kwenda lugha ya pili ambayo ni lugha ya Kiswahili. Watoto walio wengi wana athari ya lugha ya mama. Mapendekezo ya utafiti ni kwamba lugha ya kikonjo inaleta athari kwa Watoto wakikonjo wenyewe wanapokuwa wanajifunza lugha ya Kiswahili sanifu. Mtoto wa kikonjo akijifunza lugha ya Kiswahili tangu utotoni kitamwezesha kuimudu lugha hii ya Kiswahili sanifu.
Kiswahili kimekuwa lugha inayotumiwa katika ngazi mbalimbali za kielimu, maofisini, serikali.